
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha
Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amepokea kwa mshtuko
mkubwa na huzuni nyingi taarifa za kifo cha ghafla cha Mheshimiwa
Kepteni John Damian Komba, Mbunge wa Jimbo la Nyasa, Mjumbe wa
Halmashauri Kuu ya taifa ya CCM na msanii hodari sana wa kizazi chake.
Katika
salamu zake za rambirambi kwa Spika wa Bunge, Mheshimiwa Anne Semamba
Makinda na Katibu Mkuu wa CCM, Mheshimiwa Abdulrahman Kinana, Mheshimiwa
Kikwete amesema:
“Nimepokea
kwa mshtuko mkubwa na huzuni nyingi taarifa za kifo cha ghafla cha
Mheshimiwa Kepteni John Komba, ambacho nimejulishwa kuwa kimetokea
mchana wa leo, Jumamosi, Februari 28, 2015, kwenye Hospitali ya TMJ, Dar
es Salaam.”
Kwa
hakika, sina maneno ya kutosha kuelezea kwa fasaha hasara ambayo taifa
letu na chama chetu kimepata kutokana na kifo cha Kepteni Komba. Taifa
letu limepoteza hazina kubwa na mtu muhimu.
Nimejua
Kepteni Komba kwa muda mrefu sana, nimefanya naye kazi. Alikuwa msanii
ambaye kiwango chake cha usanii kilikuwa hakipimiki, alikuwa na sifa
kubwa za uongozi, alikuwa mpenzi, mzalendo na mtu mwaminifu sana kwa
taifa lake na katika jambo lolote aliloliamini.,”
"Ndani
ya Chama chetu, naomba salamu zangu ziwafikie wanachama wetu wote kwa
kupoteza mwanachama mwenzao, ziwafikie viongozi na hasa wajumbe wa
Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ambayo imepoteza mwakilishi mwenzao na wasanii wote wa Tanzania One Theatre (TOT) ambao Kiongozi wao ameondoka duniani,”
Naungana
na wanafamilia kuomboleza kifo cha rafiki yetu, ndugu yetu na kiongozi
mwenzetu. Napenda wanafamilia wajue kuwa natambua uchungu wao katika
kipindi hiki na tahayari yao ya kuondokewa na mhimili wa familia.
"Niko nao katika maombolezo na katika kumwomba Mwenyeji Mungu aiweke peponi roho ya Marehemu Kepteni John Damian Komba. Amen.”
0 comments :
Post a Comment